Thursday, August 30, 2012

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA BLOG YA GEORGE MARATO



Mbunge wa jimbo la Musoma vijijini Mh NIMROD MKONO akicheza ya Ritungu ambayo inachezwa na makabila ya Wakurya,Wazanaki,Wasimbiti,Wakiroba na jamii nyingine ya mkoa wa Mara hasa katika sherehe mbalimbali za heshima,hapa wananchi wa kijiji cha Mwibagi wakimpongeza mbunge huyo baada ya kujenga barabara kwaajili ya kurahisisha mawasiliano

Mwandishi mwandamizi wa ITV na Radio One George Marato akiwa nje ya ukumbi wa Bunge hivi karibuni mjini Dodoma
Mwandishi mwandamizi wa ITV na Radio One George Marato akiwa nje ya ukumbi wa Bunge hivi karibuni mjini Dodoma
Mhariri wa habari wa ITV na Radio One Stephen Chuwa mwenye vazi maalum linalovaliwa na watu wa nchi za Magharibi akiwa na mwandishi mwandamizi wa ITV na Radio One katika sherehe iliyoandalwa na mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dk Reginald Mengi kwaajili ya kujipongeza baada ya kumaliza mwaka 2011 katika ukumbi maarufu wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Baadhi ya waandishi wa habari wa ITV na Radio One wakiwa katika sherehe iliyoandaliwa na mwenyekiti wa IPP Dr Reginald Mengi,mwenye tai ni mwandishi mwandamizi George Marato mkoani Mara
Hawa ni baadhi ya maafisa wa JWTZ katika kikosi cha Makoko Musoma wakiwa katika maandalizi ya sherehe za kutimiza miaka 48 ya kuanzishwa kwa JWTZ
Kila kazi inaugumu wake huyu ni askari wa JWTZ akitoa heshima kwa Amiri jeshi mkuu Rais Jakaya Kikwete hayupo pichani wakati wa mazishi ya mkuu wa majeshi mstaafu Generali Mwita Kyaro
Hii ni moja ya barabara zinazojengwa na mbunge wa Musoma vijijini Mh NIMROD MKONO,katika kufungua mawasiliano katika jimbo lake.
Serikali ina kila sababu kuwaeleza wananchi mgodi wa Buhemba ni mali ya nani,haya ni mabaki ya mgodi huo ambao ulisababisha hasara ya zaidi ya bilioni 30 kwa wananchi wanazunguka mgodi huo
Wilaya ya Bunda imeanza kutekeleza mradi wa kuwapatia wananchi hati miliki za ardhi wananchi wake ili kuwawezesha kutumia hati hizo kukopa katika vyombo vya fedha kama njia moja wapo ya kujikomboa na umasikini
Diwani wa kata ya Buhemba,akizungumzia madhara yaliyosababishwa na uwekezaji wa mgodi wa Buhemba,hivi sasa wananchi hao wanadai zaidi ya bilioni 30 kama fidia iliyosababishwa na mgodi huo uliodaiwa ni wa jeshi kupitia kampuni ya Meremeta

No comments:

Post a Comment